61

Nimemwona Rafiki

1

Nimemwona rafiki, wa thamani kubwa, Ananipenda kwa ‘pole, kwa pendo amini, Kuishi kutengwa naye, la, huku siwezi, Tunakaa pamoja, Bwana nami.

2

Pengine ninachoka, mimi mdhaifu, Ndipo ninamtegemea, alivyoalika, Huniongoza njiani, pahali pa nuru, Twatembea pamoja Bwana nami.

3

Namweleza huzuni, mimi mdhaifu, Vile vinavyosumbua, vinavyopendeza, Huniagiza kutenda, yanayonipasa, Twatembea pamoja, Bwana nami.

4

Ajua natamani, kuwavuta watu, Hivyo ananipeleka, kutangaza Neno, Nitangaze pendo lake, kwa nini akafa, Twahubiri pamoja, Bwana nami.