63

Niuonapo Msalaba

1

Niuonapo Msalaba, Kristo aliponifia, Kwangu pato ni hasara, kiburi nakichukia.

2

Na nisijivune Bwana, ila kwa sadaka yako, Upuzi sitaki tena, zi chini ya damu yako.

3

Tazama kichwani kwake, mikononi na miguu, Huzuni pendo twaona, vyabubujika daima.

4

Vitu vyote vya dunia, si sadaka ya kutosha, Pendo zako zaniwia, nafsi mali na maisha.