1
Piga panda ya injili, onyesha watu wote, Ili anayesikia, atubu aokoke.
Kiitikio
Piga panda ya injili, uipige kwa nguvu, Mungu amekuagiza, mateka wawe huru.
2
Uipige vilimani, kwa kila tambarare, Pande zote miji yote, isikie injili.
3
Uipige mipakani, barabarani pia, Iwatangazie wote, wanaitwa na Baba.
4
Uipige watu wengi, wataka wawe huru, Waambie kwamba Yesu, asema “Njoni kwangu.”