65

Twendeni Askari

1

Twendeni askari watu wa Mungu, Yesu yuko mbele, tumwandame juu, Ametangulia Bwana vitani, twende mbele kwani ndiye amini.

Kiitikio

Twendeni askari, watu wa Mungu, Yesu yuko mbele, tumwandame juu.

2

Jeshi la Shetani likisikia, jina la Mwokozi litakimbia, Kelele za shangwe zivume pote, ndugu inueni zenu sauti.

3

Kweli kundi dogo watu wa Mungu, la watakatifu ni letu fungu, Hatutengwi nao moja imani, tumaini moja na moja dini.

4

Haya mbele watu nasi njiani, inueni mioyo nanyi sifuni, Heshima na sifa yake Mfalme. juu hata chini sana zivume.