69

Cha Kutumaini Sina

1

Cha kutumaini sina, ila damu yake Bwana, Sina wema wa kutosha, dhambi zangu kuziosha.

Kiitikio

Kwake Yesu, nasimama, Ndiye mwamba, ni salama, Ndiye mwamba, ni salama.

2

Njia yangu iwe ndefu, yeye hunipa wokovu, Mawimbi yakinipiga, nguvu zake ndiyo nanga.

3

Damu yake na sadaka, nategemea daima, Yote chini yakiisha, Mwokozi atanitosha.

4

Nikiitwa hukumuni, rohoni nina amani, Nikivikwa haki yake, sina hofu mbele zake.