7

Mungu Msaada Wetu

1

Mungu Msaada wetu, tangu miaka yote, Ndiwe tumaini letu, la zamani zote.

2

Kivuli cha kiti chako, ndiyo ngome yetu, Watosha mkono wako, ni ulinzi wetu.

3

Kwanza havijakuwako, nchi na milima, Ndiwe Mungu, chini yako twakaa salama.

4

Na miaka elfu ni kama, siku moja kwako; Utatulinda daima, tu raia wako.

5

Bwana Msaada wetu tangu miaka yote, Mlinzi wetu na ngome, daima, milele.