74

Niambie Ee Mlinzi

1

Niambie Ee mlinzi, je, kumepambazuka , Utukufu wa Zayuni, pana dalili zake? Msafiri uondoke, utazame mbinguni, Kiunoni ujifunge, ni kucha alfajiri.

2

Mlinzi, inamulika, nuru njiani mwako, Dalili za kuja kwake, kwamba siku karibu, Panda itakapolia, itawaamsha wafu, Watakatifu wa Mungu, kuwapa kutokufa.

3

Mlinzi ione nuru, ya mwaka wa Sabato, Sauti zinatangaza, ufalme ni karibu, Msafiri ninaona, mlima wa zayuni, Mji wa Yerusalemi, nayo fahari yake.

4

Kwenye mji wa dhahabu, anaketi Mfalme, Katika kiti kizuri, huku anatawala, Pana amani po pote, mashamba husitawi, Na ardhi ina rutuba; mito ni mitulivu.

5

Mlinzi twakaribia, nchi iliyo nzuri, Twende mbele tufurahi, nchi inachangamka, Sikieni kuna wimbo, wa waliookoka, Kaza mwendo ujiunge, na kundi kubwa hili.