1
Mpaka lini Bwana, utakaa mbali? Kumetuchosha moyo, kukawia hivi, Utatujia lini, ili tufurahi, Katika ile nuru, kuja kutukufu?
2
Mpaka lini Yesu, utaacha watu, Uliowakomboa, wawe na mashaka? Wachache waamini, kwamba utarudi, Wachache wa tayari, Bwana kukulaki.
3
Waamshe watu wako, tangaza ujumbe, “Mwe watakatifu, Bwana yu karibu,” Utatujia lini, ili tufurahi, Katika ile nuru, kuja kutukufu?