1
Jua la rohoni mwangu, mpendwa Mwokozi wangu, Usiku giza hapana, ukiwa karibu Bwana.
2
Nikipata usingizi, nijaze fikara hizi, Ni tamu sana, nilale pendoni mwako milele.
3
Kaa nami ewe Bwana, usiku kama mchana, Nisiishi mbali nawe, ni uhai kuwa nawe.
4
Kama mtoto mnyonge, ameshawishwa atange, Mtafute ewe Bwana, ujirudishie tena.
5
Wagonjwa wape amani, waneemeshe maskini, Waliao, Mtulizi, wape wote usingizi.
6
Asubuhi tutokapo, tukaribie tulipo, Twingiapo duniani, tuwe mwako mkononi.