1
Po pote mashamba yajaa, tele nafaka pevu, Po pote yang’aa meupe, bondeni na nyandani.
Kiitikio
Mwenye mavuno twasihi, upeleke wavuni, Wayakusanye mazao, hata kazi yaishe.
2
Wapeleke uchaoni, waende na jotoni, Hata jua lishukapo, wakusanye ko kote.
3
Enyi wakazi wa bwana, yaleteni mazao, Na jioni ingieni, kwake na furaha kuu.