1
Twende kwa Yesu mimi nawe, njia atuonya tuijue, Imo chuoni na mwenyewe, hapa asema njoo,
Kiitikio
Na furaha tutaiona, mioyo ikitakata sana, Kwako Mwokozi kuonana, na milele kukaa.
2
“Wana na waje,” atwambia, furahini kwa kusikia, Ndiye Mwokozi wetu hasa, na tumtii njoni.
3
Wangojeani? Leo yupo, sikiza sana asemapo, Huruma zake zitwitapo, ewe kijana njoo.